Kuendesha na Bolt Tanzania

Tunatafuta madereva wenye magari ili wajiunge na kuendesha na Bolt. Ili kuendesha na Bolt Tanzania, tafadhali hakikisha umefikisha mahitaji kama yalivyo orodheshwa hapa chini:

Mahitaji ya chombo cha usafiri

  • Modeli ya gari lazima iwe ya mwaka 1998 au  mpya zaidi
  • Modeli ya pikipiki lazima iwe ya mwaka  2005 au mpya zaidi
  • Modeli ya Bajaji lazima iwe ya mwaka 2005 au mpya zaidi.

Nyaraka zinazohitajika

  • Picha
  • Pasipoti au kadi ya kitambulisho
  • Leseni ya Udereva
  • Kadi ya Usajili wa Chombo cha Usafiri
  • Bima ya chombo cha usafiri
  • Hati ya tabia njema (inayopatikana wizara ya mambo ya ndani).

Nyaraka za ziada kwa ajili ya Bajaji, Boda na Gari

  • Leseni ya Latra
  • Leseni ya TRA.

Kamilisha hatua zifuatazo kujiunga na kuendesha nasi:

  • Hatua ya kwanza: Jiunge mtandaoni ili kuanza mchakato wa kujisaliji
  • Hatua ya pili: Pakia  nyaraka na taarifa zako
  • Hatua ya tatu: Hudhuria mafunzo na kisha akaunti yako itasajiliwa.

Kumbuka: Vyombo vya usafiri vinathibitishwa ndani ya masaa 2-6 baada ya kukusanywa.

Request in seconds, ride in minutes.

Available for iOS and Android devices.
Request in seconds, ride in minutes.