VAT kwenye Kamisheni
Hii inafuata kodi ya huduma za kidigitali iliyopendekezwa kulingana na kanuni za NTSA. Masharti ya Kanuni za VAT (Utoaji wa Soko la Kielektroniki, Kimtandao na Kidigitali), 2023 yanalazimisha Bolt kukusanya na kulipa VAT ya asilimia 16 inayotozwa kwenye Kamisheni ya Bolt ya asilimia 18.
Kamisheni ya Bolt haizidi asilimia 18. Asilimia hii 18 haitajumuisha VAT kulingana na kanuni za NTSA. Tozo itakuwa kiwango cha asilimia 16 kwenye ada ya kamisheni kwa kila safari
Kuanzia tarehe 1 Aprili, 2025
Kanuni za VAT za 2023 zinaweka majukumu kwa watoaji wa huduma kwenye masoko ya kidigitali, lakini madereva bado wana wajibu wa kodi ya mapato. Inashauriwa sana madereva kutafuta ushauri kutoka KRA au mtaalamu wa kodi ili kuhakikisha wanafuata sheria za kodi za Kenya kikamilifu.
Maswali ya Jumla
Pakia picha ya leseni halali ya dereva kwenye wasifu wako kisha wasilisha tiketi kupitia wasifu wako wa dereva kwa kubofya hapa.
Wasilisha tiketi kupitia wasifu wako wa dereva kwa kubofya hapa.
Kama dereva, una chaguo la kuunganisha na usafiri ambao tayari upo kwenye jukwaa la Bolt au kusajili usafiri mpya wa kuendesha ukiwa na hati zinazohitajika.
Tazama video kwa mwongozo wa hatua kwa hatua wa kuwasilisha ombi lako la kuunganisha kupitia Jukwaa la Dereva.
Kuunganisha kunachukua masaa machache. Epuka kuwasilisha maombi mengi ili tuweze kukufikia haraka iwezekanavyo.
Maswali Yanayoulizwa Sana kuhusu Leseni ya Udereva
Kuhuisha leseni ya udereva mtandaoni ni haraka zaidi ukishalipa.
Haya ni masharti ya msingi ili uweze kuendesha na Bolt. Madereva wapya ni lazima pia wapate leseni ya udereva ili kujisajili kuwa Dereva wa Bolt. Kisheria, unaweza kukabiliwa na faini ya hadi KES 20,000 au kifungo cha miezi 3 kwa kosa la kwanza na faini ya hadi KES 30,000 au kifungo cha miezi 6 au vyote viwili kwa makosa mfululizo.
Hali hii ikiwa imetokea, utahitaji kuomba leseni mpya ya kidigitali kwenye Jukwaa la TIMS la
NTSA kama ifuatavyo:
- Ingia kwenye Jukwaa la TIMS la NTSA
- Chagua leseni ya udereva
- Chagua "Omba leseni ya kidigitali ya udereva"
- Jaza maelezo yanayohitajika
- Lipa ada inayohitajika na utembelee Ofisi ya NTSA ukiwa na ankara yako na picha ya pasi.
- Chukua leseni yako ya udereva kwa wakati ulioainishwa.
Matangazo kwenye Usafiri
Peleka usafiri wako kwa Gimco Limited, Barabara ya Kiambere, Upperhill. Siku za wiki: 3 asubuhi - 11 jioni Jumamosi: 3 asubuhi - 7 mchana
Bolt italipa gharama za matangazo na ada za leseni za kaunti.
- Mapato yanategemea idadi ya safari unazofanya kila wiki.
- Kamilisha safari 45 na upate hadi KES 1,650 za ziada kila wiki.
- Kamilisha safari 55 na upate hadi KES 2,000 za ziada kila wiki.
- Kamilisha safari 65 na upate hadi KES 2,350 za ziada kila wiki.
- Utasalia kuwa sehemu ya promosheni ya matangazo kwa kipindi cha miezi 12, isipokuwa iwe imehuishwa.
- Bolt itafanya ukaguzi wa kimwili au pepe wa ubora wa usafiri wenye matangazo ya Bolt kila mwezi.
- Unahitajika kukamilisha safari 45 kwa wiki ili ustahili fidia ya matangazo.
- Huwezi kuwa na stika za matangazo za washindani kwenye usafiri wako wenye matangazo ya Bolt.
- Mwishoni mwa kipindi cha promosheni ya matangazo, au mkataba ukasitishwa na moja ya pande zote, utachukua jukumu la kuondoa stika ya matangazo ya Bolt isipokuwa promosheni ikiwa imehuishwa.
Tembelea Ukurasa wetu wa Kimataifa wa Matangazo kwenye Usafiri wa Dereva kwa taarifa zaidi.
Kuweka stika kunachukua chini ya saa moja kwa wastani, kwa hivyo utarudi barabarani na kupata mapato tena ndani ya muda mfupi.
Hapana. Muonekano wa asili utabaki salama ikiwa stika zitawekwa na kuondolewa kwa kitaalamu na washirika wetu wanaoaminika.
Pata pesa kwa kuendesha na Bolt
Kuwa dereva wa Bolt, weka ratiba yako na pata pesa kwa kuendesha!
Kuwa bosi wako mwenyewe. Anza kuendesha na kupata pesa!
Inachukua dakika 2 tu kuwasilisha taarifa zako.
